Psalms 29

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba

(Zaburi Ya Daudi)


1 aMpeni Bwana, enyi mashujaa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.

2 bMpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3 cSauti ya Bwana iko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.


4 dSauti ya Bwana ina nguvu;
sauti ya Bwana ni tukufu.

5 eSauti ya Bwana huvunja mierezi;
Bwana huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.

6 fHufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
Sirioni
Yaani Mlima Hermoni.
urukaruke kama mwana nyati.

7 hSauti ya Bwana hupiga kwa miali
ya umeme wa radi.

8 iSauti ya Bwana hutikisa jangwa;
Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.

9 jSauti ya Bwana huzalisha ayala,
na huuacha msitu wazi.
Hekaluni mwake wote wasema,
“Utukufu!”


10 k Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;
Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.

11 l Bwana huwapa watu wake nguvu;
Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
Copyright information for SwhKC